Majazi - Printable Version +- MyElimu (https://myelimu.com) +-- Forum: GENERAL STUDENTS DISCUSSIONS (https://myelimu.com/forum-general-students-discussions) +--- Forum: KISWAHILI (https://myelimu.com/forum-kiswahili) +--- Thread: Majazi (/thread-majazi) |
Majazi - MwlMaeda - 06-14-2017 Majazi ni mbinu ya mhusika kuwa na jina lake rasmi (jina la kuzaliwa) linaloambatana na tabia/mienendo/sifa zake. Aidha, majazi inaweza kuwa mbinu ya sanaa. Mhusika Bahati katika riwaya; ikiwa maisha yake yatadhihirisha kuwa na bahati nyingi; basi hiyo itakuwa ni mbinu ya Majazi. Mzee Tumbo Kubwa anapenda kula sana kana kwamba hashibi. Neema ni msichana mzuri, mpole, mpenda amani Mganga Kuzimu ni mganda hodari sana anayeongoza ibada za gizani katika kijiji cha Mizukani RE: Majazi - francissmtambo - 06-16-2017 Mwalimu hapa chini sijaelewa (mganga kuzimu ni mganda) Neno mganda Lina maana gani?? Sent from my Phantom6-Plus using MyElimu mobile app (06-14-2017, 05:53 PM)MwlMaeda Wrote: Majazi ni mbinu ya mhusika kuwa na jina lake rasmi (jina la kuzaliwa) linaloambatana na tabia/mienendo/sifa zake. Aidha, majazi inaweza kuwa mbinu ya sanaa.Neno mganda Lina maana gani?? Sent from my Phantom6-Plus using MyElimu mobile app RE: Majazi - MwlMaeda - 06-18-2017 francissmtambo;1573 Wrote:Mwalimu hapa chini sijaelewa (mganga kuzimu ni mganda) Neno mganda Lina maana gani?? Nimerekebisha neno mganda ni mganga |