0
TANGA RUDI MASOMONI.
Keti kitini nikweleze, hukohuko Ngamiani,
Kwa tungo nikuongoze, pakawe sawa kitwani,
Moro usiichokoze, 'takutokea puani,
Tanga rudi masomoni.
Msimbe usimbeze, alikushinda dimbani,
Ngoma yake usiteze, nakushauri mwendani,
Itakuja ikulize, uwe hoi taabani,
Tanga rudi masomoni.
Ninajuwa nikujuze, kutunga ni yangu fani,
Jaribu nikupoteze, upotee duniani,
Ama vipi jisogeze, nikutie darasani,
Tanga rudi masomoni.
Tanga usijikweze, kama kujuwa zamani,
Sasa sinieleze, kuwa ungali fanani,
Mbinu zote umalize, hunifiki abadani,
Tanga rudi masomoni.
Huku Moro sikatize, saiziyo Mombasani,
Kwa hivyo sijitokeze, na kutaka ushindani,
Sitake nikukimbize, kwa bakora hadharani,
Tanga rudi masomoni.
Mja sijiheleleze, na kujitia shidani,
Hata fanya jiongeze, kwa kuenda ugangani,
Tungo ili zipendeze, vema uzame kinani,
Tanga rudi masomoni.
Huko kwenu uwajuze, Kinyonga hawezekani,
Tena wasijiingize, kunifata uwanjani,
Aula wajitulize, waepushe tafarani,
Tanga rudi masomoni.
(JIBU)
TANGA NI CHUO CHA FANI
Rangimoto jitulize, kisha utwae uneni
Goti'chi ulipigize, nikufunze kwa yakini
Elimu ukasambaze, wendapo kwenu nyumbani
Tanga ni chuo cha fani
Nyakangao muulize, Salimu Kibao nani
Na akupe habarize, Jimbi Pera Ridhiwani
Siyo sauti upaze, mithili ya majinuni
Tanga ni chuo cha fani
Jituze mwana jituze, u mchanga kwenye fani
Ngoma hino usicheze, humudu shindo la beni
Ukisema ucheleze, usijejuta mbeleni
Tanga ni chuo cha fani
Ushairi nikujuze, asili yake ni pwani
Kirangacho ukipoze, Morogoro mji duni
Bure sijiangangize, kutaka jipa thamani
Tanga ni chuo cha fani
Unataka uongoze!, eti ushike sukani
Kwa tungo ipi tujuze, nitazamapo sioni
Njoo tukutengeneze, Tanga ndiyo malishoni
Tanga ni chuo fani
La shamba sijipumbaze, huwezi wika mjini
Wagamba nisikatize, hasa kwa kuhofu nini
Nitapita nikujuze, nenda Dodoma chuoni
Tanga ni chuo cha fani
Naacha kupiga zeze, karibu chuo cha fani
Ni Tanga na wilayaze, njoo upate auni
Utunzi tukukoleze, kwa jaala ya Manani
Tanga ni chuo cha fani
Karibu: www.mwalimuwakiswahili.com
Keti kitini nikweleze, hukohuko Ngamiani,
Kwa tungo nikuongoze, pakawe sawa kitwani,
Moro usiichokoze, 'takutokea puani,
Tanga rudi masomoni.
Msimbe usimbeze, alikushinda dimbani,
Ngoma yake usiteze, nakushauri mwendani,
Itakuja ikulize, uwe hoi taabani,
Tanga rudi masomoni.
Ninajuwa nikujuze, kutunga ni yangu fani,
Jaribu nikupoteze, upotee duniani,
Ama vipi jisogeze, nikutie darasani,
Tanga rudi masomoni.
Tanga usijikweze, kama kujuwa zamani,
Sasa sinieleze, kuwa ungali fanani,
Mbinu zote umalize, hunifiki abadani,
Tanga rudi masomoni.
Huku Moro sikatize, saiziyo Mombasani,
Kwa hivyo sijitokeze, na kutaka ushindani,
Sitake nikukimbize, kwa bakora hadharani,
Tanga rudi masomoni.
Mja sijiheleleze, na kujitia shidani,
Hata fanya jiongeze, kwa kuenda ugangani,
Tungo ili zipendeze, vema uzame kinani,
Tanga rudi masomoni.
Huko kwenu uwajuze, Kinyonga hawezekani,
Tena wasijiingize, kunifata uwanjani,
Aula wajitulize, waepushe tafarani,
Tanga rudi masomoni.
(JIBU)
TANGA NI CHUO CHA FANI
Rangimoto jitulize, kisha utwae uneni
Goti'chi ulipigize, nikufunze kwa yakini
Elimu ukasambaze, wendapo kwenu nyumbani
Tanga ni chuo cha fani
Nyakangao muulize, Salimu Kibao nani
Na akupe habarize, Jimbi Pera Ridhiwani
Siyo sauti upaze, mithili ya majinuni
Tanga ni chuo cha fani
Jituze mwana jituze, u mchanga kwenye fani
Ngoma hino usicheze, humudu shindo la beni
Ukisema ucheleze, usijejuta mbeleni
Tanga ni chuo cha fani
Ushairi nikujuze, asili yake ni pwani
Kirangacho ukipoze, Morogoro mji duni
Bure sijiangangize, kutaka jipa thamani
Tanga ni chuo cha fani
Unataka uongoze!, eti ushike sukani
Kwa tungo ipi tujuze, nitazamapo sioni
Njoo tukutengeneze, Tanga ndiyo malishoni
Tanga ni chuo fani
La shamba sijipumbaze, huwezi wika mjini
Wagamba nisikatize, hasa kwa kuhofu nini
Nitapita nikujuze, nenda Dodoma chuoni
Tanga ni chuo cha fani
Naacha kupiga zeze, karibu chuo cha fani
Ni Tanga na wilayaze, njoo upate auni
Utunzi tukukoleze, kwa jaala ya Manani
Tanga ni chuo cha fani
Karibu: www.mwalimuwakiswahili.com