06-10-2017, 12:33 PM
0
KUKU KITOWEO MURUA KWA WALAJI!!!
Ukipita sokoni ukawakuta kuku wakiwa kwenye *tenga* jaribu kuwatizama mara mbili mbili kisha jiulize maswali kibao!.
Ulipowatizama umewaona wakiwa na huzuni au furaha?.
✍Kwa utafiti niliofanya katika masoko mengi nimewakuta kuku wakiwa _wamechangamka sana!, na hasa kama wakiwa wamewekewa chakula wanachokipenda sana!
✍Kuku wengine _hufikia hatua ya kugombana kutokana na chakula walichowekewa katika tenga lile!!
✍Wakati mwingine nimewahi kushuhudia _majogoo yenye nguvu yakionesha ubavu kwa majogoo dhaifu na pengine hata kuyatia kashikashi yasile chochote kilicholetwa pale tengani!
✍Jambo jingine kubwa nilio liona _ni majogoo yenye nguvu kujimilikisha majike yote yalioko kwenye tenga lile!, huku majogoo dhaifu yakiumia kwa kukosa haki yao ya kimsingi!
[/b]?Hayo ni mambo makubwa manne ambayo mimi na wewe tumewahi kuyaona mubashara kwa kuku wa tengani!, lakini _*je, tumewahi kujiuliza maswali na kupata ibra ya matukio hayo?
*Ibra ya kwanza!*: Hawa _kuku wote walioko tengani, bila kujali jogoo wala jike, wooote maadamu wako tengani hawako huru_. Wakilifahamu hilo ni hatua nzuri!
*Ibra ya Pili!* : Yale majogoo yenye nguvu yanapaswa kuelewa kwamba _hata yenyewe hayako salama bali ni kitoweo murua kinachosubiri wanunuzi tu!!!_. Yakifahamu hili ni hatua nzuri!
*Ibra ya tatu!*: Yale majogoo yenye nguvu _yatumie nguvu yalizonazo sio kuwapiga kuku wenzao bali kujinasua na kuwanasua wengine kutoka kwenye tenga ili yasiwe kitoweo!!!_ Yakifahamu hili ni hatua nzuri!
*Ibra ya nne!*: Kuku wote wanapaswa kufahamu kwamba _huduma nzuri wanazofanyiwa wakiwa kwenye tenga si ishara ya huruma na mapenzi ya dhati dhidi yao_. Hilo wakilifahamu ni hatua nzuri!.
*Ibra ya tano!:*. Wale kuku dhaifu wanapaswa kuelewa kwamba _uhuru sahihi waliokosa hautokani na yale majogoo yanayojifaragua kwenye tenga!!!_. Wakilifahamu hili ni hatua nzuri!
Ukipita sokoni ukawakuta kuku wakiwa kwenye *tenga* jaribu kuwatizama mara mbili mbili kisha jiulize maswali kibao!.
Ulipowatizama umewaona wakiwa na huzuni au furaha?.
✍Kwa utafiti niliofanya katika masoko mengi nimewakuta kuku wakiwa _wamechangamka sana!, na hasa kama wakiwa wamewekewa chakula wanachokipenda sana!
✍Kuku wengine _hufikia hatua ya kugombana kutokana na chakula walichowekewa katika tenga lile!!
✍Wakati mwingine nimewahi kushuhudia _majogoo yenye nguvu yakionesha ubavu kwa majogoo dhaifu na pengine hata kuyatia kashikashi yasile chochote kilicholetwa pale tengani!
✍Jambo jingine kubwa nilio liona _ni majogoo yenye nguvu kujimilikisha majike yote yalioko kwenye tenga lile!, huku majogoo dhaifu yakiumia kwa kukosa haki yao ya kimsingi!
[/b]?Hayo ni mambo makubwa manne ambayo mimi na wewe tumewahi kuyaona mubashara kwa kuku wa tengani!, lakini _*je, tumewahi kujiuliza maswali na kupata ibra ya matukio hayo?
*Ibra ya kwanza!*: Hawa _kuku wote walioko tengani, bila kujali jogoo wala jike, wooote maadamu wako tengani hawako huru_. Wakilifahamu hilo ni hatua nzuri!
*Ibra ya Pili!* : Yale majogoo yenye nguvu yanapaswa kuelewa kwamba _hata yenyewe hayako salama bali ni kitoweo murua kinachosubiri wanunuzi tu!!!_. Yakifahamu hili ni hatua nzuri!
*Ibra ya tatu!*: Yale majogoo yenye nguvu _yatumie nguvu yalizonazo sio kuwapiga kuku wenzao bali kujinasua na kuwanasua wengine kutoka kwenye tenga ili yasiwe kitoweo!!!_ Yakifahamu hili ni hatua nzuri!
*Ibra ya nne!*: Kuku wote wanapaswa kufahamu kwamba _huduma nzuri wanazofanyiwa wakiwa kwenye tenga si ishara ya huruma na mapenzi ya dhati dhidi yao_. Hilo wakilifahamu ni hatua nzuri!.
*Ibra ya tano!:*. Wale kuku dhaifu wanapaswa kuelewa kwamba _uhuru sahihi waliokosa hautokani na yale majogoo yanayojifaragua kwenye tenga!!!_. Wakilifahamu hili ni hatua nzuri!